Machapisho

Judith Mbilinyi - Maisha Yangu Official Video

Picha
Bwana Yesu Asifiwe!  Mpendwa msomaji wa blog yetu pendwa ya GOSPEL HEADLINES LEO, leo kwa uwezo wa Mungu nimekusogezea video ya wimbo wenye baraka nyingi sana uitwao Maisha Yangu  kutoka kwa mwimbaji mahiri wa nyimbo za injili  kutoka jijini Dar es salaam Tanzania anayefahamika kwa jina la Judith Mbilinyi. Wimbo huu wa kuabudu umetayaarishwa katika studio za  EM Records  chini ya mikono thabiti ya mtayarishaji Erasto Augustino. Hii ni moja kati ya nyimbo zenye mafuta ya pekee sana ya upako katika kumwabudu Mungu ambaye kupitia Bwana wetu Yesu Kristo ameachilia nguvu ya ajabu kwa mtumishi Judith Mbilinyi ambaye kupitia wimbo huu ameonekana kuwa katika uwepo wa kipekee wa Mungu akilisifu jina la Yesu Kristo na kuzikumbusha nafsi zetu pia kuwa maisha yetu yapo mikononi mwa Bwana wetu Yesu.  Ili kuutazama wimbo huu ambao upo kwa mfumo wa video, bofya hapo chini. Karibu sana. Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Judith Mbilinyi  kupitia: Simu ...

WAIMBAJI: TUNDUMA KUMEKUCHA KWA YESU

Picha
WAIMBAJI: TUNDUMA KUMEKUCHA KWA YESU. Na Mwandishi wetu,   SONGWE,  Umoja wa waimbaji wa nyimbo za injili mkoa wa Mbeya na Songwe, kwa pamoja umeendelea kushika hatamu kwa kile kinachoelezwa kuwa NGUVU YA USHIRIKIANO imeishibisha huduma ya uimbaji iliyomo ndani ya vipawa vya waimbaji hao. Umoja huo ambao hadi sasa unakadiriwa kuwa na jumla ya waimbaji takribani 200, ambao licha ya kuwa na huduma ya mmoja mmoja lakini umeendelea kushirikiana katika kuifanya huduma hii ikiwa ni pamoja na kuandaa mikutano, mikesha na makongamano yenye lengo la kujifunza neno la Mungu pamoja na wakristo wengine mahali popote.   Kwa kulitambua dhumuni la Umoja huo na kwa kutambua jukumu la kila mwimbaji anayehusisha umoja huo na kwa kutambua umuhimu wa kumtumikia Kristo aliye tumaini letu, viongozi wa kamati kuu tendaji ya Mkoa wa Mbeya kwa niaba ya waimbaji, wameratibu maandalizi ya Kongamano kubwa la neno la Mungu litakalo fanyika Mkoa wa Songwe-Tunduma mnamo tarehe 16...

KILIO CHA YATIMA

Nickson Mahundi - Kilio cha Yatima (Official Video) Machi 03, 2018  KILIO CHA YATIMA    Haleluya mpendwa msomaji wa blog yetu pendwa ya GOSPEL HEADLINES LEO . Leo nimekusogezea wimbo uitwao KILIO CHA YATIMA. Wimbo huu ulioimbwa na mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka nchini Tanzania, NICKSON MAHUNDI umebeba kusudi la kuwatetea watoto yatima na wote waishio katika mazingira hatarishi, ambao wamekosa malezi na huduma mbalimbali za kiafya na kijamii. Mwimbaji huyu ambaye pia ni mwanahabari na mtangazaji mahiri, amefanyika faraja sana katika maisha ya watoto yatima na hasa waishio maisha ya mtaani.    Licha ya huduma yake ya uimbaji na utangazaji lakini pia NICKSON MAHUNDI ni 'Managing director' wa kituo cha utangazaji cha Redio Best Fm  90.3 mHZ kilichopo Mkoani Njombe, Wilaya ya Ludewa.    Nikukaribishe kuitazama video hii kwa moyo mmoja, naamini utajifunza kitu kupitia ujumbe huu wenye harufu ya ...

MAHOJIANO MAALUM NA EV. MHUGO HANTISH

Picha
TAZAMA MAHOJIANO HAPA CHINI Hello mpenzi msomaji wetu wa GOSPEL HEADLINES LEO, bila shaka ukheri wa afya kabisa. Kama ilivyo  ada kukuletea habari za wainjiishaji na injili kutoka ndani na nje ya Tanzania, leo tumekusogezea karibu yako mahojiano maalum ya Ev. Mhugo Hantish akiwa na mtangazaji wa kipindi cha FARAJA YAKO, Getrude Mwakatobe wa Radio Bomba Fm 104.1 Mbeya. PICHA KWA HISANI YA HINJU ZE ONE, DH     TANGAZO JE, UNAHITAJI KUTANGAZA HABARI YAKO HAPA   www.hantishmhugo.blogspot.pe ? KAMA NI "NDIO" TUTUMIE EMAIL YAKO KWENDA   hantishmhugo@gmail.com   AU UJUMBE/PIGA/WHATSAPP 0768788303 . gospelheadline@2018 " The voice to the voiceless "

Mr. Marco Mnanago - Usilie Mama (Official Audio)

Picha
Na Mwandishi Wetu. IRINGA. Habari yako mpenzi msomaji wetu wa GOSSPEL HEADLINES LEO? Ni siku nyingine tena iliyochukua nafasi maishani mwetu ambapo leo tunamleta kwenu mwimbaji wa nyimbo za injili aitwaye Mr.MARCO MINANAGO kutoka mkoani Iringa, ambaye leo anautambulisha rasmi wimbo wake hapa GOSPEL HEADLINES LEO. Wimbo uitwao USILIE MAMA umetengenezwa katika studio za 2Star Records katika mikono bora ya mtayarishaji Kay B.    Akizungumza na GOSPEL HEADLINES LEO, Minanago amesema "wimbo huu wa USILIE MAMA umekua na maana kubwa sana kwangu kwasababu mama ni jeshi kubwa. Hivyo nimemtumia mama ili kutuwakilisha sote ya kwamba hatutakiwi kukata tamaa tupatwapo na majaribu."   Akiongeza zaidi, Mr Marco amesema "hakuna haja ya kulia hadi tukamkufuru Mungu hasa pale tunapopatwa na mitihani ya maisha. Ikiwa subira yavuta heri basi kuna kila sababu ya kusubiri na kuvumilia kwakua Mungu wetu yupo kwaajili yetu na atatusaidia kwa majira na wakati wake....